TAPO Logo

TAPO Logo

Wednesday, May 24, 2006

Wanyama

WANYAMA
Duniani kuna aina nyingi sana ya viumbe kama vile ndege, wanyama, samaki, wadudu na wengineo, na viumbe wote hao wanatabia , maumbile,mahitaji mapendo na mifumo mbalimbali ya kuendesha maisha mbali ya msaada wa binadamu kwa asili ya maisha ya viumbe wa duniani. Pia kuna wanyama ambao wana akali ya kutambua na kufanya vitu mbalimbali karibia kabisa na binadamu, na sifa kubwa zaidi kwa viumbe wengi ni kuwa wanalea na kuwatunza watoto wao.


Haki za Wanyama

Nini maana ya haki za wanyama?

Haki za wanyama maana yake wanyama wana aina Fulani ya kufikirika, kuthaminika—kufikirika, kuthaminika kutokana na nini bora kwa mapenzi, mahitaji, na maamuzi yao kutokujali kama hawasikii, wanatumiwa na binadamu, au wanakaribia kutoweka na kutokajali kama wanatunzwa na binadamu {kama ilivyo kwa binadamu aliyepungukiwa na akili anaayo haki hata kama watu wote hawampendi} ina maana kutambua kuwa wanyama siyo wetu kwa ajili ya chakula, kuvaa, kiburudisho, au majaribio ya kisayansi.

Ni Haki Zipi za Wanyama ?
Wanyama wanahaki ya kuthamiwa kwa maamuzi yao wenyewe kwa mfano, mbwa ana maamuzi ya kutokuwa na maumivu anayoyapata pasipo kuwa na sababu yeyote ile, maana, kwa hiyo tunalazimika kuchukua maamuzi yao katika kuwathamini na kuwajali mbwa kuwa na haki ya kutokuwa na maumivu yasiyo ya lazima anayoyapata.

Hata hivyo wanyama kawida hawana haki zinazofanana na binadamu, kwa sababu maamuzi na mahitaji yao kawida hayafanani na yetu, na baadhi ya haki zinaweza kuwa kinyume na maisha ya wanyama, kwa mfano, mbwa hana maamuzi, hafahamu haki ya kupiga kura na kwa hiyo hana haki ya kupiga kura, tangu hapo haki hiyo itakuwa haina maana kwa mbwa na kama ilivyo kwa mtoto.

Umesimama Wapi?
Kuna baadhi ya bianadamu ambao kwa huruma na upendo wanaweza kusimama na kumtoa jongoo barabarani na kumpeleka sehemu salama. Kujali matatizo na kuwajibika ni maadili yanayopanuka na tunalazimika kuishi kila siku kwa kuhukumu na kuhukumu kuamua kila kitu kinachotokea kwa ubaya na uzuri kama tunavyoweza.

Hatuwezi kuzuia mateso yote, lakini haina maana kuwa hatuwezi kuzuia mateso yeyote katika maisha ya sasa ya duniani yenye muenekano wa mapungufu ya uchaguzi, kawaida huwa kuna huruma na ubabe, njia ambazo wengi wetu tunazotumia katika kula, kuvaa, kuburudika, na kujifunza sisi wenyewe kuliko kuua wanyama.



Vipi Miti na Mimea?
Hakuna njia inayoonyesha tuamini kuwa miti na mimea inahisi maumivu, kwani haina mishipa ya fahamu “ubongo”na mwisho wa mishipa ya fahamu. Sababu pekee inayoonyesha kuwa wanyama wanahisi maumivu ni jinsi watakavyo jihami.
iwapo utashika kitu ambacho kitakuumiza au kujeruhi, maumivu yatakufundisha kutokugusa na kukiacha pekee siku nyingine. Tangu hapo miti na mimea haiwezi kutembea kuepuka maumivu na hivyo haitaji kijifunza kuepuka baadhi ya vitu.

Imani Katika Haki Za Wanyama
Ni vizuri kuamini katika haki za wanyama kwani kila mtu anawajibika katika maamuzi yake, lakini “uhuru wa kufikiri” kawaida huwa hauwendani na “uhuru wa kutenda”. Upo huru kuamini chochote unachotaka ingawaje huwaumizi wengine, unaweza kuamini kuwa wanyama ni lazima wauwawe, kwamba watu weusi ni lazima wawe watumwa, au mwanamke ni lazima apigwe, lakini hufanyi imani yako uiweke kwenye majaribio- yaani kwa kutenda.

Wanyama hawazielewi haki zao, mara nyingi hawaheshimu haki zetu, je ni kwanini tunatoa mawazo yetu ya kiroho juu yao?
Kwa sababu wanyama kushindwa kufahamu na kuingia katika miongozo yetu ni sawasawa na mtoto mdogo au kichaa kushindwa kufana hivyo. Wanyama hawako, hawana, au hawajawezeshwa kuchagua kubadilishwa tabia zao, lakini binadamu anayo akili ya kuchagua kati ya tabia zinazowaumiza wengine na kutokuwaumiza wengine.

Ni vigumu kuepuka kutesa wanyama na mara nyingi hufanyika bila kufahamu?
Ni kweli ni vigumu kuishi maisha yako bila ya kuleta majeruhi kwa viumbe wote, kwa bahati mbaya tumeshakanyaga siafu na viumbe wengine, lakini haina maana kuwa tumedhamilia kuwakanyaga siafu hao. Lakini kwa sababu unaweza kusababisha ajali kwa kumgonga mtu na gari haina maana kumfanya bianadamu awe ni kwa ajili ya kugongwa na gari.

Vipi kuhusu mila, tamaduni, na kazi zinazotegemea kutumia wanyama?
Uanzishaji wa magaari, uzuiaji wa biashara ya utumwa, na mwisho wa vita kuu ya pili ya dunia kulilazimisha kutokea na mifumo mingine ya kufanya kazi na kuiendeleza. Hii ilikuwa ni chachu katika maendeleo jamii za binadamu—siyo sababu ya kuvuruga maendeleo.

Wanyama wengi wanaotumika kwa chakula, kazi, manyoya, ngozi na majaribio ya kisayansi wamezaliwa kwa ajili hiyo?
Kwa kuzaliwa kwa shughuli hiyo hakuwewzi kubadilisha uwezo wa kibaolojia wa mnyama kusikia maumivu na huzuni.

Mungu ameweka wanyama hapa duniani kwa ajili ya kuwatawala, vitabu vya dini vimetupa utawala juu wanyama?

Kutawala siyo sawasawa na kutawala kwa mabavu na utesaji, mfano, Rais wa Tanzania anatawala au anawaongoza watanzania, lakini haina maana kuwa anaweza kuwala au kuwatesa watanzania. Iwapo tunatawala wanyama, ukweli kabisa ni kuwalinda, siyo kuwatumia kwa mahitaji yetu. Hakuna chochote kwenye vitabu vya dini kinachoweza kuelezea maisha yetu ya sasa na mipangilio ambayo inaharibu mazingira, kuharibu na kutokomeza vizazi vya wanyama wa porini na vifo vya wanyama kila mwaka.

Je ni kweli wanyama wanaofungiwa muda wowote hawateseki kwa sababu hawajui kitu chochote kile?
Kuzuiwa kufanya karibia vitu vyote vya asili kitabia kunasababisha maumivu au usumbufu wa hali ya juu hata kama mnyama amefungiwa tangu azaliwe anahitaji kutembea, kugusana pamoja kunyoosha miguu yao au mabawa yao na mazoezi. Wanyama wanaochungwa, na wanyama wanaotembea kikundi huwa wanapata kuchanganyikiwa wakati watakapoishi kwa kutenganishwa au watakapowekwa kwenye makundi makubwa ambapo wanashindwa kutambuana.

Iwapo utumiaji wa wanyama ungekuwa ni makosa ingekuwa ni uvunjaji wa sheria?
Utawala wa sheria siyo kinga ya imani ya kiroho, nania ametenda kosa na nani hakutenda kosa kisheria huamuliwa na maoni na mapendekezo ya wanasheria wa sasa, sheria zinabadilika kama mapendekezo ya jamii au mabadiliko katika siasa yatabadilika, lakini maadili hayabadilki. Angalia baadhi ya vitu ambavyo kwa wakati Fulani ilikuwa ni sheria dunia ajira ya mtoto, utumwa wa binadamu, na ukandamizwaji wa wanawake.

Wanyama hawana akili au wameendelea kama binadamu?
Kuwa na uwezo na akili nyingi hakumaanishi binadamu mmoja kumnyanysa mwingine kwa malengo yake, kwanini binadamu mwenye akili anyanyase wasio kuwa bindamu. Kuna wanyama ambao wana akili, wabunifu, wanaojali, wanaowasiliana na wenye uwezo wa kutumia lugha kuliko baadhi ya bianadamu , kama ilivyo kwa sokwe mtu akilinganishwa na mtoto mchanga au kichaa wa hali ya juu sana, je itakuwa wanyama wenye akili kuwa na haki na binadamu wenyekili kidogo kunyimwa haki?