TAPO Logo

TAPO Logo

Friday, July 21, 2006

Kunguru

KUNGURU
Kunguru wa Zanzibar


Jina la kisayansi anajulikana Kama “corvus splendens”

Historia yake katika Tanzania:

Kunguru hawa Kwa mara ya kwanza walipelekwa katika visiwa vya Zanzibar kutoka katika mji wa Bombay na serikali ya India mwaka 1891 mara baada ya kuombwa na Sir Gerald portal. Waliletwa kunguru 50 Kwa ajili ya kudhibiti uchafu na takataka zinazoweza kuliwa na ndege hawa katika sehemu ijulikanayo kama “Stone Town.”
Ulipofika mwaka 1917 uzalianaji wa kunguru uliongezeka sana na kufanya waonekane kama ndege waharibifu sehemu ya stone town. Kunguru Siyo tu wanadhibiti takataka zinazooza tu, Bali pia wanakula wanyama wadogowadogo (Kama panya), mazao ya mbegu, matunda na mazao mengine.

Lakini pia kunguru wanashindana na aina nyingi za viumbe tofauti kwa chakula. na katika sehemu za viota vya ndege moja kwa moja wanakula vifaranga na mayai kutoka kwa ndege wengine. Huu ni ukweli kuwa sehemu ambayo wanapatikana kunguru, ndege wametengeneza viota sehemu ambayo kunguru hatofikia, na siyo rahisi kukuta ndege amejenga kiota kwenye mti, tofauti na sehemu ambayo hakuna kunguru utakuta ndege wamejenga kiota kwenye miti na sehemu nyingine ya wazi kabisa.

Utambuzi

Kuna aina sita (6) ya kunguru duniani, na kunguru ni huyu wa Zanzibar ndiye kunguru mdogo kuliko wengine katika jamii Yao [sm 43]. Ana rangi nyeusi ikitapakaa sehemu kubwa ya mwili na rangi ya majivu kwenye shingo na kifuani, wana macho ya kahawia wakiwa wakubwa.
Vifaranga vya kunguru vinafafana na kunguru wakubwa, lakini wana macho meusi na mdomo wa ndani huwa unakuwa na rangi ya pink.

Chakula chao

Kunguru wana aina nyingi ya chakula,
Chakula chao ni pamoja na:
Mbegu- karanga, mahindi nk
Matunda
Wadudu
Wanyama wadogo wadogo
Mayai
Mizoga, nk.

Uzaaji wao.

Kunguru ni jamii ya ndege, na hutengeneza kiota kikubwa kilicho na umbile kama la bakuli, kwa kutumia vijiti, majani, magome ya miti na manyoya. Kiota hujegwa kwa ushirikiano wa kunguru dume na jike, mayai hulaliwa na jike tu, na kifaranga mmoja huzaliwa kwa mwaka, kifaranga hulishwa na dume na jike

Kusambaa Kwa kunguru.

Kutokana na jinsi kunguru wanavyozaliana kwa wingi na upatikanaji wa chakula chao kwa urahisi, ndivyo polepole wanavyozidi kutapakaa sehemu tofauti za nchi ya Tanzania. Kwa mfano, mkoani Morogoro utaona kunguru mmoja mmoja katika manispaa ya morogoro, lakini baada ya miaka michache watakuwa wengi Sana. na inasadikika kuwa kutokana na kunguru kuweza kuishi kwenye hali ya hewa tofauti, basi katika miaka ijayo Mikoa yote ya Tanzania watapatikana.

Wednesday, July 19, 2006

International Day of Action for Korean Dogs and Cats

This year's global day of action, co-sponsored by Korean animal protection groups CARE and KAAP, will be held on July 20th, 2006, to coincide with the first of Korea's "Bok days" (literally, the hot, dog days of summer). South Korea's dog meat consumption increases during this time of year because some superstitiously believe they can keep cool by eating animals who do not sweat.

Last year, IDA and AFK successfully organized activists from a dozen countries - including Argentina, Belgium, Canada, Columbia, Ireland, Mexico, Peru, Russia, South Korea, Spain and Tanzania - for this international day of protest. In the U.S., demonstrators converged on Korean consulates and embassies in New York City; Washington, D.C.; Atlanta, Ga.; San Francisco and Los Angeles, Calif.; and Portland, Ore. to oppose the illegal eating of cats and dogs in South Korea.

The international press covered the protests favorably in several newspapers and online news websites. In Seoul, South Korea, dozens of protestors rallied the public against dog and cat consumption with colorful signs, costumes and inventive tactics like locking themselves in small cages dressed as dogs. In San Francisco, 20 people came to IDA's protest at the Korean Consulate and a good number brought their companion dogs to be ambassadors for their exploited canine cousins in Korea. In the few short weeks leading up to the demonstration, activists collected over 5,000 petition signatures, which were presented to the Korean Consulate at the protest.

Tuesday, July 18, 2006

TWIGA

TWIGA


Twiga: Giraffe: Giraffe Camelopardalis
Wanapatikana: Africa, Kusini mwa jangwa la Sahara, kwenye miti ya
Wazi Na kwenye majani.
Urefu mpaka mapembe: Dume, mita 4.7-5.3, jike mita 3.94-5
Uzito: Dume, kilo 800- 1930, jike, kilo 550-1180
Tabia: Wanajitenga kimakundi
Umri wa kuishi: Miaka 25 wakiwa porini
Chakula chao: Majani kutoka juu ya miti, majani ya kwenye vichaka,
Mizizi nk.
Sauti: Kawaida huwa kimya, lakini wanapiga chafya, mtoto hulia
Kama atachanganyikiwa.

Kuna subspecies tisa za twiga zinazotambulika, zote zinafanana lakini zinatofautiana kwa michirizi ya rangi, na mgawanyiko wa kijiografia.
Twiga ni viumbe wastaarabu, lakini hawajiweki kwenye makundi, badala yake wanakutana kimakundi kila siku, lakini mchanganyiko wa kundi unatofautiana kila siku baada siku. Twiga dume wa sehemu Fulani huwa anaanzisha hali ya kusachi kwa kurefusha shingo.Iwapo dume mgeni ataingia makazi ya dume mwingine atafukuzwa na dume lenye makazi yake, na wote wawili watagombana kwa kugonganisha vichwa vyao mpaka mmoja wao atakaposhindwa. Fuvu la dume twiga ni gumu zaidi kwa sababu hiyo.

Uzaaji: kubalehe Kwa twiga jike Ni kati ya miezi 48-60, twiga dume Ni miezi 42. Twiga wanapandana wakati wowote Kwa mwaka Na mimba kubebwa kati ya siku 450-464. Huwa kunakuwa Na mtoto mmoja anayezaliwa, mapacha ni adimu kuzaliwa.
Twiga jike katika msimu huwatamanisha madume yaliyo karibu naye, lakini Ni dume mkumbwa tu ndiye anayeshinda. Dume lililoshinda huwafukuza madume wadogo Kwa kuwatisha: kupigana, siyo lazima katika hali hii. Mimba ya twiga huishia miezi 15 baada ya hapo huzaa Na mama Na mtoto wa twiga watakwenda sehemu au uwanja wa ushirikiano unaotumiwa Na majike muda kwa muda na mtoto wake tu hapo. Watoto wa twiga wanazaliwa Na mapembe, ambayo siyo kawaida. Mapembe yanalala kwenye fuvu la mtoto wakati wa kuzaliwa, lakini yatajinyoosha mara baada ya wiki kwanza kuzaliwa .
Uwanja wa kutunzia watoto huwa kuna kuwa na mtoto mdogo wa twiga kila mara ataachwa na watoto wenzie wenye kufikia umri sawa wakati mama yake atakapo kwenda kutafuta chakula wakati katikati ya siku. Hata hivyo watoto wa twiga wanawindwa Sana na fisi, chui na mbwa mwitu, na ni nusu yao ndio tu watakao pona katika muda wa miezi sita ya kwanza.
Jinsi mtoto anavyokuwa mkubwa atajiunga na mama kwenda kutafuta chakula. Simba ndio adui Yao mkubwa, lakini twiga anauwezo wa kumuua simba iwapo Kama atamsukuma kwa nguvu kwa kutumia miguu yake ya mbele. Baada ya watoto wa twiga kufikisha umri wa mwaka mmoja ni wachache kati ya mmoja kwa kumi atakufa kwa mwaka.
Kujitegemea kwa twiga kunachukua miezi 15 ingawa mama yake atakutana tena na dume miezi 5 baada ya mtoto kuzaliwa, twiga kijana wa kike anakaa na mama yake, lakini twiga kijana wa kiume atakwenda kujiunga na umoja wa madume wote na kwenda kutembea peke yake atakapofikisha umri kiasi cha miaka 3.

Chakula: Twiga ni wanyama wanaokula majani na hula majani miti na vichaka. Wanatofautiana katika ukusanyaji wa chakula na kutegemea na nini anacho kula.
Baadhi ya miti Kama vile acacia, ina miba mingi Sana, hivyo twiga anahitaji kuwa makini wakati atakapokuwa ana kula chakula kutoka kwenye miti hiyo. Huwa wanamega majani na mikungu ya majani na kuwacha miiba pekee Yao. Ulimi wa twiga unaweza kufikia sm 45 kwa urefu, na hutumia kusukuma majani ndani ya mdomo na kupaka chakula chote kwa mate yanayovutika kufanya chakula kiwe rahisi kumeza.
Jinsi twiga wanavyotumia kutafuta na kukifikia chakula inapunguza ushindani katika jinsia. Twiga jike ana inama chini ili kufikia matawi ya majani ya chini na vichaka, lakini twiga dume anarefusha shingo yake kufikia majani ya juu ya miti. Twiga jike anakula mpaka kufikia masaa 12 katika kila masaa 24, lakini dume linakula muda mchache. Dume linakula kiasi cha kilo 60 za majani Kwa siku.

Uhifadhi wa twiga
Twiga ni mnyama aliye ma mvuto katika kumwangalia na hata jinsi anavyotembea kwa mwendo wa madaha kutokana na urefu wake ambapo kuanzaia kichwa, shingo, mwili na hata mguu inavyotingishika
Ili twiga na vizazi vyake vijavyo waweze kuishi pasipo bughudha ya binadamu popote pale ndani ya nchi ya Tanzania na majirani zake, tunahitaji kuwa na huruma na upendo na kuheshimu viumbe hawa kwa kuwasaidia kwa hali yeyote watakapo patwa na jambo lolote la kutishia uhai wao, ikiwa pamoja na kuzuia ujangili na uwindaji, utumiaji wa bidhaa zitokanazo na twiga, kuhifadhi na kulinda mazingira ya wanyama hawa wanayoishi, kama vile kutokuchoma moto mapori, kutupa kitu chochote kile kitakachowadhuru mwili na uhai wao kwa ujumla, na kuwalinda kutopata magonjwa.

Wednesday, July 12, 2006

Hali Bora kwa Wanyama

HALI BORA KWA WANYAMA


Hali bora kwa Wanyama wanaotumiwa na Binadamu inatokana na jinsi ya kukubaliana na mfumo wa maisha bila ya kuteseka kwenye mazingira yaliyotayarishwa na binadamu.

Wanasayansi na Wanafilosofia wanatambua kuwa Wanyama wana akili ya kuendeshea maisha yao na hata hali ya mwili {afya na utambuzi wa mwili} ambavyo vinaweza kudhuliwa kwa jinsi gani Binadamu wanavyowatendea na kuwahifadhi.

Aina Tano za uhuru zinatumika kuelezea mahitaji yote ya Wanyama wa kufugwa na wajibu wa kuwatunza kama ifuatavyo;
Uhuru wa kutokuwa na maumivu, majeraha na magonjwa.
Uhuru wa kutokuwa na njaa, kiu, na utapiamlo.
Uhuru wa kuonyesha tabia ya kawaida.
Uhuru wa kutokutishwa na kutokusumbuliwa.
Uhuru wa kutokukosa raha ya mwili

Aina Tano za uhuru zinaweza kufikiwa kwa mfano,
Kuwatayari kuwapatia uwezekano wa maji safi ya kunywa, chakula bora cha kujenga afya ya mwili,na katika hali ambayo wanyma wamepewa chakula kwa kipimo, kufanya uwezekano wa kupatikana aina nyingine ya chakula kama vile majani ili kumridhisha mnyama
Kumpatia mazingira bora ambayo ni pamoja na kimvuli, nyumba ya kuishi, na sehemu nzuri ya kupumzikia.
Kuzuia na katambua haraka na kutibu magonjwa na majeraha, kumpatia chanjo pale inapobidi, kudhibiti mzunguko wa sehemu bora ya malisho ili kupunguza maambukizi ya magonjwa,
Mnyama apatiwe nusu kaputi haraka pale ambapo matibabu yataleta maumivu ya muda mrefu {kwa mfano kuvnjika kwa miguu}. Usimsafirishe mnyama mwenye majeraha au ugonjwa,au mnyama aliyefikia hatua za mwisho za ujauzito, labda iwe unampeleka kwa mganga wa mifugo au kwenye matibabu yenye faida kwa mnyama{kwamba usimsafirishe mnyama wa aina hiyo kwenye machinjio au sehemu myingine ambayo mwisho wake ni kuchinjwa }