TAPO Logo

TAPO Logo

Thursday, December 07, 2006

Ngozi za Wanyama na Utamaduni Tanzania


Makabila mengi yanatumia bidhaa nyingi zitokanazo na wanyama katika mila na utamaduni wao, lakini kitendo hicho bado ni ukatili wa wanyama, ingekuwa vizuri pia wangetumia ngozi ya binadamu.

Konokono-----east african Land Snails


Thursday, November 16, 2006

Makazi Ya Viumbe


Makaza ya viumbe wengin hasa warukao hutegemea hasa kuishi kwenye miti na majani kwa kipindi chao chote cha maisha yao.
Baadhi ya watu wamekuwa wakikata miti hovyo na kuchoma majani kila sehemu ya nchi yetu na kitendo hiki ni ukatili wa hali ya juu kwa viumbe hao, watu wanatakiwa kuwa na huruma na kufikiria kila jambo wanalotenda

Humane Education


Humane Education is key factor for decreasing violence among young people, we need to educates young peoples to understand and to care about human being and animal, that all are creatures and need the right to live.
Teaching humane education in Tanzania is not famous despite the peace song the country leaders speaking, if we can teach all people concerning the caring of others we can keep the country of Tanzania in more safe nation to live in the world

Saturday, November 11, 2006

Make Donation

Please make donation to our organization in order to make us works by donating anything through the following address
Tanzania Animals Protection Org
Box 62921
Dar es salaam
Tanzania
Email;tap_org@yahoo.com
Tell; +255 0756 027419

Thursday, November 02, 2006

Mateso ya Ng'ombe Pugu Mnadani

Wanyama aina ya Ng'ombe katika mnada wa pugu wanateswa sana kiasi kwamba inatia shaka katika jamii ya watanzania kuwa wengi kati yetu wanawatendea wanyama vibaya sana na kuonyesha kuwa wanajali pesa tu kuliko kuwapatia hali bora wanyama hao hata kama wanachinjwa.
Tunahitaji msaada mkubwa wa kukabiliana na tatizo hili kwa yeyote yule Tafadhali wasiliana nasi kwa simu 0756 027419 au email tap_org@yahoo.com


Friday, September 08, 2006

World Farm Animals Day 2006

World Farm Animals Day 2006
Information Table, Exhibit, Ads, Web BannerDate/Time: 29 Sept -1 Oct Location: Ubungo Riverside Features: We will show through media and other work will take place at our office Ubungo Riverside Dar es salaam

Tapo tutafanya maonyesho kidogo yanayohusu siku ya wanyama duniani kupitia vyombo vya habari kuanzia tarehe 29 September mpaka tarehe 3 October 2006, na yeyote anakaribishwa kutembelea katika ofisi yetu iliyokoUbungo River side Dar es salaam , ili uje kupata elimu kuhusiana wanyama na viumbe wengine katika kuwahudumia katika wema na upendo

Friday, August 25, 2006

Kahama Donkeys

Support Kahama Donkeys




Donkeys at District of Kahama in Shinyanga Province are in bad conditions due to health poor condition, bad designing of carts and careless of owners, most of them are puling carts with sores on necks.

National Farmers Day Nanenane- Arusha 2006






Maonyesho ya sikukuu ya wakulima Kitaifa 2006 yalifanyika mkoani arusha Katika viwanja vya Themi njiro, TAPO tulishiriki kikamilfu katika kuelimisha jamii kuhusiana na masula mbalimbali yanayohusu haki za wanyama na viumbe wote kwa ujumla, lengo letu lilikuwa kuelimisha na wala siyo kufanya biashara kama washiriki wengine walivyofanya.

Friday, July 21, 2006

Kunguru

KUNGURU
Kunguru wa Zanzibar


Jina la kisayansi anajulikana Kama “corvus splendens”

Historia yake katika Tanzania:

Kunguru hawa Kwa mara ya kwanza walipelekwa katika visiwa vya Zanzibar kutoka katika mji wa Bombay na serikali ya India mwaka 1891 mara baada ya kuombwa na Sir Gerald portal. Waliletwa kunguru 50 Kwa ajili ya kudhibiti uchafu na takataka zinazoweza kuliwa na ndege hawa katika sehemu ijulikanayo kama “Stone Town.”
Ulipofika mwaka 1917 uzalianaji wa kunguru uliongezeka sana na kufanya waonekane kama ndege waharibifu sehemu ya stone town. Kunguru Siyo tu wanadhibiti takataka zinazooza tu, Bali pia wanakula wanyama wadogowadogo (Kama panya), mazao ya mbegu, matunda na mazao mengine.

Lakini pia kunguru wanashindana na aina nyingi za viumbe tofauti kwa chakula. na katika sehemu za viota vya ndege moja kwa moja wanakula vifaranga na mayai kutoka kwa ndege wengine. Huu ni ukweli kuwa sehemu ambayo wanapatikana kunguru, ndege wametengeneza viota sehemu ambayo kunguru hatofikia, na siyo rahisi kukuta ndege amejenga kiota kwenye mti, tofauti na sehemu ambayo hakuna kunguru utakuta ndege wamejenga kiota kwenye miti na sehemu nyingine ya wazi kabisa.

Utambuzi

Kuna aina sita (6) ya kunguru duniani, na kunguru ni huyu wa Zanzibar ndiye kunguru mdogo kuliko wengine katika jamii Yao [sm 43]. Ana rangi nyeusi ikitapakaa sehemu kubwa ya mwili na rangi ya majivu kwenye shingo na kifuani, wana macho ya kahawia wakiwa wakubwa.
Vifaranga vya kunguru vinafafana na kunguru wakubwa, lakini wana macho meusi na mdomo wa ndani huwa unakuwa na rangi ya pink.

Chakula chao

Kunguru wana aina nyingi ya chakula,
Chakula chao ni pamoja na:
Mbegu- karanga, mahindi nk
Matunda
Wadudu
Wanyama wadogo wadogo
Mayai
Mizoga, nk.

Uzaaji wao.

Kunguru ni jamii ya ndege, na hutengeneza kiota kikubwa kilicho na umbile kama la bakuli, kwa kutumia vijiti, majani, magome ya miti na manyoya. Kiota hujegwa kwa ushirikiano wa kunguru dume na jike, mayai hulaliwa na jike tu, na kifaranga mmoja huzaliwa kwa mwaka, kifaranga hulishwa na dume na jike

Kusambaa Kwa kunguru.

Kutokana na jinsi kunguru wanavyozaliana kwa wingi na upatikanaji wa chakula chao kwa urahisi, ndivyo polepole wanavyozidi kutapakaa sehemu tofauti za nchi ya Tanzania. Kwa mfano, mkoani Morogoro utaona kunguru mmoja mmoja katika manispaa ya morogoro, lakini baada ya miaka michache watakuwa wengi Sana. na inasadikika kuwa kutokana na kunguru kuweza kuishi kwenye hali ya hewa tofauti, basi katika miaka ijayo Mikoa yote ya Tanzania watapatikana.

Wednesday, July 19, 2006

International Day of Action for Korean Dogs and Cats

This year's global day of action, co-sponsored by Korean animal protection groups CARE and KAAP, will be held on July 20th, 2006, to coincide with the first of Korea's "Bok days" (literally, the hot, dog days of summer). South Korea's dog meat consumption increases during this time of year because some superstitiously believe they can keep cool by eating animals who do not sweat.

Last year, IDA and AFK successfully organized activists from a dozen countries - including Argentina, Belgium, Canada, Columbia, Ireland, Mexico, Peru, Russia, South Korea, Spain and Tanzania - for this international day of protest. In the U.S., demonstrators converged on Korean consulates and embassies in New York City; Washington, D.C.; Atlanta, Ga.; San Francisco and Los Angeles, Calif.; and Portland, Ore. to oppose the illegal eating of cats and dogs in South Korea.

The international press covered the protests favorably in several newspapers and online news websites. In Seoul, South Korea, dozens of protestors rallied the public against dog and cat consumption with colorful signs, costumes and inventive tactics like locking themselves in small cages dressed as dogs. In San Francisco, 20 people came to IDA's protest at the Korean Consulate and a good number brought their companion dogs to be ambassadors for their exploited canine cousins in Korea. In the few short weeks leading up to the demonstration, activists collected over 5,000 petition signatures, which were presented to the Korean Consulate at the protest.

Tuesday, July 18, 2006

TWIGA

TWIGA


Twiga: Giraffe: Giraffe Camelopardalis
Wanapatikana: Africa, Kusini mwa jangwa la Sahara, kwenye miti ya
Wazi Na kwenye majani.
Urefu mpaka mapembe: Dume, mita 4.7-5.3, jike mita 3.94-5
Uzito: Dume, kilo 800- 1930, jike, kilo 550-1180
Tabia: Wanajitenga kimakundi
Umri wa kuishi: Miaka 25 wakiwa porini
Chakula chao: Majani kutoka juu ya miti, majani ya kwenye vichaka,
Mizizi nk.
Sauti: Kawaida huwa kimya, lakini wanapiga chafya, mtoto hulia
Kama atachanganyikiwa.

Kuna subspecies tisa za twiga zinazotambulika, zote zinafanana lakini zinatofautiana kwa michirizi ya rangi, na mgawanyiko wa kijiografia.
Twiga ni viumbe wastaarabu, lakini hawajiweki kwenye makundi, badala yake wanakutana kimakundi kila siku, lakini mchanganyiko wa kundi unatofautiana kila siku baada siku. Twiga dume wa sehemu Fulani huwa anaanzisha hali ya kusachi kwa kurefusha shingo.Iwapo dume mgeni ataingia makazi ya dume mwingine atafukuzwa na dume lenye makazi yake, na wote wawili watagombana kwa kugonganisha vichwa vyao mpaka mmoja wao atakaposhindwa. Fuvu la dume twiga ni gumu zaidi kwa sababu hiyo.

Uzaaji: kubalehe Kwa twiga jike Ni kati ya miezi 48-60, twiga dume Ni miezi 42. Twiga wanapandana wakati wowote Kwa mwaka Na mimba kubebwa kati ya siku 450-464. Huwa kunakuwa Na mtoto mmoja anayezaliwa, mapacha ni adimu kuzaliwa.
Twiga jike katika msimu huwatamanisha madume yaliyo karibu naye, lakini Ni dume mkumbwa tu ndiye anayeshinda. Dume lililoshinda huwafukuza madume wadogo Kwa kuwatisha: kupigana, siyo lazima katika hali hii. Mimba ya twiga huishia miezi 15 baada ya hapo huzaa Na mama Na mtoto wa twiga watakwenda sehemu au uwanja wa ushirikiano unaotumiwa Na majike muda kwa muda na mtoto wake tu hapo. Watoto wa twiga wanazaliwa Na mapembe, ambayo siyo kawaida. Mapembe yanalala kwenye fuvu la mtoto wakati wa kuzaliwa, lakini yatajinyoosha mara baada ya wiki kwanza kuzaliwa .
Uwanja wa kutunzia watoto huwa kuna kuwa na mtoto mdogo wa twiga kila mara ataachwa na watoto wenzie wenye kufikia umri sawa wakati mama yake atakapo kwenda kutafuta chakula wakati katikati ya siku. Hata hivyo watoto wa twiga wanawindwa Sana na fisi, chui na mbwa mwitu, na ni nusu yao ndio tu watakao pona katika muda wa miezi sita ya kwanza.
Jinsi mtoto anavyokuwa mkubwa atajiunga na mama kwenda kutafuta chakula. Simba ndio adui Yao mkubwa, lakini twiga anauwezo wa kumuua simba iwapo Kama atamsukuma kwa nguvu kwa kutumia miguu yake ya mbele. Baada ya watoto wa twiga kufikisha umri wa mwaka mmoja ni wachache kati ya mmoja kwa kumi atakufa kwa mwaka.
Kujitegemea kwa twiga kunachukua miezi 15 ingawa mama yake atakutana tena na dume miezi 5 baada ya mtoto kuzaliwa, twiga kijana wa kike anakaa na mama yake, lakini twiga kijana wa kiume atakwenda kujiunga na umoja wa madume wote na kwenda kutembea peke yake atakapofikisha umri kiasi cha miaka 3.

Chakula: Twiga ni wanyama wanaokula majani na hula majani miti na vichaka. Wanatofautiana katika ukusanyaji wa chakula na kutegemea na nini anacho kula.
Baadhi ya miti Kama vile acacia, ina miba mingi Sana, hivyo twiga anahitaji kuwa makini wakati atakapokuwa ana kula chakula kutoka kwenye miti hiyo. Huwa wanamega majani na mikungu ya majani na kuwacha miiba pekee Yao. Ulimi wa twiga unaweza kufikia sm 45 kwa urefu, na hutumia kusukuma majani ndani ya mdomo na kupaka chakula chote kwa mate yanayovutika kufanya chakula kiwe rahisi kumeza.
Jinsi twiga wanavyotumia kutafuta na kukifikia chakula inapunguza ushindani katika jinsia. Twiga jike ana inama chini ili kufikia matawi ya majani ya chini na vichaka, lakini twiga dume anarefusha shingo yake kufikia majani ya juu ya miti. Twiga jike anakula mpaka kufikia masaa 12 katika kila masaa 24, lakini dume linakula muda mchache. Dume linakula kiasi cha kilo 60 za majani Kwa siku.

Uhifadhi wa twiga
Twiga ni mnyama aliye ma mvuto katika kumwangalia na hata jinsi anavyotembea kwa mwendo wa madaha kutokana na urefu wake ambapo kuanzaia kichwa, shingo, mwili na hata mguu inavyotingishika
Ili twiga na vizazi vyake vijavyo waweze kuishi pasipo bughudha ya binadamu popote pale ndani ya nchi ya Tanzania na majirani zake, tunahitaji kuwa na huruma na upendo na kuheshimu viumbe hawa kwa kuwasaidia kwa hali yeyote watakapo patwa na jambo lolote la kutishia uhai wao, ikiwa pamoja na kuzuia ujangili na uwindaji, utumiaji wa bidhaa zitokanazo na twiga, kuhifadhi na kulinda mazingira ya wanyama hawa wanayoishi, kama vile kutokuchoma moto mapori, kutupa kitu chochote kile kitakachowadhuru mwili na uhai wao kwa ujumla, na kuwalinda kutopata magonjwa.

Wednesday, July 12, 2006

Hali Bora kwa Wanyama

HALI BORA KWA WANYAMA


Hali bora kwa Wanyama wanaotumiwa na Binadamu inatokana na jinsi ya kukubaliana na mfumo wa maisha bila ya kuteseka kwenye mazingira yaliyotayarishwa na binadamu.

Wanasayansi na Wanafilosofia wanatambua kuwa Wanyama wana akili ya kuendeshea maisha yao na hata hali ya mwili {afya na utambuzi wa mwili} ambavyo vinaweza kudhuliwa kwa jinsi gani Binadamu wanavyowatendea na kuwahifadhi.

Aina Tano za uhuru zinatumika kuelezea mahitaji yote ya Wanyama wa kufugwa na wajibu wa kuwatunza kama ifuatavyo;
Uhuru wa kutokuwa na maumivu, majeraha na magonjwa.
Uhuru wa kutokuwa na njaa, kiu, na utapiamlo.
Uhuru wa kuonyesha tabia ya kawaida.
Uhuru wa kutokutishwa na kutokusumbuliwa.
Uhuru wa kutokukosa raha ya mwili

Aina Tano za uhuru zinaweza kufikiwa kwa mfano,
Kuwatayari kuwapatia uwezekano wa maji safi ya kunywa, chakula bora cha kujenga afya ya mwili,na katika hali ambayo wanyma wamepewa chakula kwa kipimo, kufanya uwezekano wa kupatikana aina nyingine ya chakula kama vile majani ili kumridhisha mnyama
Kumpatia mazingira bora ambayo ni pamoja na kimvuli, nyumba ya kuishi, na sehemu nzuri ya kupumzikia.
Kuzuia na katambua haraka na kutibu magonjwa na majeraha, kumpatia chanjo pale inapobidi, kudhibiti mzunguko wa sehemu bora ya malisho ili kupunguza maambukizi ya magonjwa,
Mnyama apatiwe nusu kaputi haraka pale ambapo matibabu yataleta maumivu ya muda mrefu {kwa mfano kuvnjika kwa miguu}. Usimsafirishe mnyama mwenye majeraha au ugonjwa,au mnyama aliyefikia hatua za mwisho za ujauzito, labda iwe unampeleka kwa mganga wa mifugo au kwenye matibabu yenye faida kwa mnyama{kwamba usimsafirishe mnyama wa aina hiyo kwenye machinjio au sehemu myingine ambayo mwisho wake ni kuchinjwa }



Saturday, June 03, 2006

Mateso ya Ng'ombe

Mateso ya Ng'ombe ndani ya nchi ni makubwa sana, je wahusika wanasemaje kwa hali ya wanyama kuwa ya mateso katika usafri?

Upendo wa Punda

Upendo Kwa Punda
Punda ni Mnyama Mstaarabu, Mtulivu na mwenye akili, na ni kiungo muhimu sana kaika kusaidia shughuli nyingi za maisha ya baadhi ya binadamu.

Punda ni mnyama rafiki sana kwa binadamu kwani anatabia ya kukubali kufuata matakwa ya binadamu. Kwa ujumla ni mnyama mwenye upendo wa hali ya juu sana

Punda anapatikana sehemu nyingi ndani ya nchi yetu ya Tanzania, na watu wengi sana wanawatumia punda katika shughuli za Kilimo, Ujenzi na hata Usafirishaji.

Pia ikumbukwe kuwa Bindamu ni mnyama, ana hisia za maumivu, ndivyo hivyohivyo kwa punda kuhisi maumivu

Kuwa na punda halafu humpatii chakula cha kutosha, kumtibu na kumuangalia afya yake ipasavyo, kumbebesha na kumvutisha mizigo yenye uzito mkubwa ni Ukatili wa hali ya juu sana, na ni uvunjaji wa sheria za haki za wanyama Tanzania.

Kitendo cha kuona punda wako ana vidonda shigoni au sehemu nyingine yeyote ya mwili na, bado unamtumia kufanya shughuli yako kupitia vidonda vyake ni Utesaji na Ukatili wa hali ya juu sana.

Ushauri wa Huruma

Muhudumie punda wako kwa huruma, upendo na heshima kwa kufuata kanuni, taratibu na sheria za nchi
Punda kwa ajili ya kuvuta au kubeba mizigo ni lazima wawe na umri kati ya miaka 4 na 25
Punda kwa ajili ya kubeba na mwenye uzito wa kilo 160 ni lazima asibebe zaidi ya kilo 50.
Punda wa kuvuta asivute kupitia shingoni, avute kupitia kifuani na mpunguzie maumivu kwa kumvalisha sponji nene au kitu kingine chochote laini
Punda wa kubeba mpunguzie maumivu kwa kumuwekea sponji, canvass au kitu kingine chochote laini.
Mchunguze punda wako kila siku kuona kama ana matatizo ya kiafya kwa kumpeleka au kumwita mganga wa mifugo.
S.L.P 62921 Dar es Salaam,

Mradi wa Kuwasiadia Punda- Kahama

Mradi wa Kuwasaidia Punda

“Hali Bora na Afya Bora”

Msimazi wa Mradi; Yohana Js Kashililah
Walengwa; Wakazi wa Wilaya ya Kahama na Punda wao
Tarehe ya kuanzia; September, 2006



1. Maelezo ya Mradi

Shirika la Hiari la Kutetea Haki za Wanyama Lijulikanalo kwa jina la TAPO yaani Tanzania Animals Protection Organization, litabeba jukumu la mradi wa kuwasidia punda katika wilaya ya kahama.
Wilaya ipo umbali wa kilomita zipatazo 221 kutoka Shinyanga Mjini katika Tanzania Bara iliyo ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Walengwa ni wakazi wa wilaya ya kahama pamoja na punda wao katika kata zote 34 yenye ongezeko la watu wapatao 679.829, asilimia kubwa ya wakaazi wote wanamiliki punda, na ndio watakaohusiswa katka kuhamisishwa kujali hali bora na afya bora za punda wao katika kata zao.

Kuna idadi ya punda wanaokadiliwa kufikia 3428 katika wilaya yote ya kahama {kutokana na ripoti ya idadi ya mifugo wilayani kahama 2001}, isiyokuwa na huduma za kituo cha afya ya mifugo. Asilimia kubwa ya wakazi wote wanajishughulisha na kilimo, na asilimia kubwa ya wakulima wanamiliki au wanamtumia mnyama aitwaye punda na wanyama wengine katika shughuli zao za kila siku, na kuna kati ya punda mmoja mpaka wanne kwa familia moja.

Punda wanatambulika kama watendaji,watoa huduma, na wanaofaa katika kusaidia ukuaji wa uchumi kwa ajili ya kukabiliana na mkakati wa kupunguza umaskini miongoni mwa jamii ya watu wa kahama, kwa ufupi punda ni muhimu katika usafiri na kazi za kilimo.

Mkokoteni wenye kuwa na mti mkubwa mmoja na punda wawili waliofungwa kwenye shingo, punda wanabeba uzito kwa kuvuta mkokoteni kupitia kwenye shingo zao nyembamba zilivofungwa kamba.

Uzito wote wa kuvuta mkokoteni unategemea shingo ya punda ambayo kutokana na uvutaji huo punda hupata maumivu makubwa na majeraha makubwa, kamba mara kwa mara zinaingilia uwezo wa kupumua.
Na hii ndiyo sababu kubwa inayowanyima raha punda na kuwaletea vidonda vikubwa.


Uwezo wa ubebaji wa punda kahama ni wa kuzidi na kuwatisha kuliko uwezo wa punda wa ubebaji wa kawaida.
Wanabeba mizigo kupita kiasi, kubeba asilimia 100 zaidi ya uzito wa mwili wao kwa umbali mrefu, uzito wote kuwa sehemu moja bila ya kuwa ya kuwa na aina ya Kilinganisho, ambapo baadhi ya watu wanambebesha punda mizigo kwa upande mmoja kwa kutumia kamba au kitu kingine chochote, hii inaweka mgandamizo mkubwa katika uti wa mgongo, mara kwa mara wanaanguka njiani, kwa muda mrefu wanakuwa na njaa na kiu.


Punda wengi wanafugwa kwa ajili ya usafiri, kama ni kwa ajili ya kubeba au kuvuta mkokoteni- kupitia madhumuni ya kusafirisha mazao ya mashambani, kuni, maji, mbolea, kukodisha, vifaa vya ujenzi kama vile mchanga, mawe, kokoto, saruji na shughuli nyingine

Usafirishaji wa mazao na shughuli zote za kilimo ndio unaongoza kwa wakulima kutumia punda wakati wa msimu wa kupanda na kuvuna kata nyingi wilayani kahama, ambapo mashamba yapo umbali wa kilomita kadhaa kutoka katika makazi ya wakulima, inachukua kiasi cha masaa manane kwa siku, na hata wakati wa usiku utakuta punda bado wapo kazini, wakipita kwenye njia yenye mawe, kwenye mabonde na milima.

Utengenezaji mbaya wa mkokoteni na ufungaji kwa punda ni tatizo kubwa linalosababisha majereha mengi kwa punda wa kahama, ambapo punda wanavuta mkokoteni kwa kutumia shingo badala ya kifua.

Hali za punda wengi ni wa kahama ni dhaifu kuanzia muonekano wa mwili mpaka mpangilio wa kiafya, wengi wana majeraha kwenye shingo,kifua,mkiani,katika miguu,usoni, kwato zina majeraha na zimeongezeka zaidi

Wamiliki wa punda wanawathamini punda wao kwa ajili ya kufanya kazi tu siyo kuwathamini katika hali bora na afya bora, hivyo mradi huu unalengo la kutoa elimu kwa wamiliki wa punda wilayani kahama kuhusiana na kuwahamasisha kuwapatia hali bora na afya bora punda wao kwa kutumia mbinu zifuatavyo;


2. Elimu na Mazoezi ya kazi

Kutakuwa na maelezo kamili katika mafunzo ya wamiliki au mtumiaji wa punda katika kutambua hali bora kwa punda, hali bora ya afya ya punda, kumzoesha punda mazoezi ya kufanya kazi, ambapo wamilki au watumiaji watawafanyisha mazoezi punda katika hali ya kutambua ni wakati gani punda wanakataa kufanya kazi zaidi.
Mafundisho mazuri yana faida kwa shughuli yote ya ufanyaji kazi iwapo itajumuisha udhibiti na utoaji amri kwa punda,na kwa kutakuwa na siku za mafunzo ya darasani kwa kila kata kama ifuatavyo

1. Elimu Kuhisiana na Malazi ya punda

Elimu hii itajumuisha kumpatia punda malazi bora yanayofaa kwa misimu yote ya hali hewa ya mwaka, kutokana na kuwa ngozi haina uwezo wa kuzuia maji- hivyo malazi bora ya punda yatamlinda katika baridi kali, na kumpatia kimvuli katika siku za joto, na kuepukana na wadudu warukao kama n’zi.

2. Elimu kuhusiana na Malisho ya Punda

Elimu hii itajumuisha wamilki au wahudumu wa punda kutambua njia gani za kumpatia malisho bora, kumlinda na majani yenye sumu na kumlinda na ugonjwa utokanao na kula kupita kiasi

3. Elimu kuhusiana na afya ya msingi ya punda

Elimu hii itajumuisha wamiliki au wahudumu wa punda kuchunguza punda kama wanaugua au wanauwezo wa kufanya kazi kwa wakati huo, au kutambua kitu chochote tofauti katika afya ya punda kabla ya kumwita mganga wa mifugo.
Kumfanyisha kazi punda asubuhi sana na jioni, kupumzisha kila mara katika kivuli na muda wa kumpatia maji, kupunguza kwato zilizoongezeka.


4. Elimu Kuhusiana na Kumtendea punda

Elimu hii itajumuisha kumtendea punda katika kuvuta mkokoteni, na ubebaji wa mizigo, jinsi gani ya kupunguza maumivu na majeraha yatokanayo shughuli nzima ya uvutaji mkokoteni kwa kuelimisha kuhusiana na utengenezaji mkokoteni usio kuwa na madhara kwa punda

3. Malengo ya Mradi

Mradi wa kuwasaidia punda wa kahama una dhamana ya kuhamasisha na kulinda afya, usalama na hali bora ya punda wote wapatikanao wilayani Kahama Mkoani Shinyanga. Miezi sita ya mradi huu itasaidia kuwasogeza wakaazi wa kahama kuwaelewa na kuwaheshimu Punda wao kama viumbe hai kwa malengo yafuatayo;
· Kubuni, kukabiliana na kuhamasisha jambo lolote linalohusiana na punda katika kuwapatia hali bora na afya bora kupitia kwa binadamu.
· Kuelewesha, kukubalika, kufufua na kuendeleza hali bora na afya bora za punda katika jamii wa watu wa kahama.

4. Umuhimu wa Mradi Huu

Ni lazima kufanya mradi huu kwa wakati uliopangwa kutokana na unyanyapaaji na unyanyasaji wa punda katika jamii ya watu wa kahama ni wa hali ya juu sana

5. Usimamizi wa Mradi

Mradi wa kusaidia punda wilayani kahama utasimamiwa kwa karibu kabisa pamoja na ushauri kutoka Kitivo cha Elimu ya Magonjwa ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine {SUA}, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo, Halamashauri ya Wilaya ya Kahama, Mganga wa Mifugo Wilaya ya Kahama, Maofisa Watendaji wa Kata, Mashirika ya Hiari, Vyombo vya Habari na Jamii kwa ujumla ili kuleta Hali Bora na Afya Bora na kutekeleza na kufanikisha malengo kamili ya mradi.
Mfumo wa usimamizi wa mradi ni;

1. Kundi la Usimamizi wa Mradi

Kundi hili linatokana na Wanachama na Wafanyakazi wa TAPO,Madaktari wa Mifugo waliofuzu na kusajiliwa, wataendeleza usimamizi wa kila siku wa shughuli za mradi, kwa kufuata ratiba ya kazi, mpangilio wa bajeti, kuhakikisha kuwa kuna mawasiliano ya kutosha pamoja na washiriki wengine wa mradi na vikundi vingine vya hiari.

2. Kundi la Ushauri la Mradi

Kundi hili linatokana na Wafadhili mbalimbali wa mradi, Wahadhili kutoka Kitivo cha Elimu ya Magonjwa ya Wanyama-Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine Morogoro {SUA}, Madaktri wa Magonjwa ya Wanyama kutoka Wizara ya Maendeleo ya mifugo, na Madaktari wa mifugo kutoka kata zote 34 za wilaya ya kahama.

Kazi za Mradi
Mradi huu unategemewa kuchukua miezi sita {6} kwa kupitia.

Kuchunguza hali iliyokuwepo

Uchunguzi kamili wa hali iliyokuwepo, afya ya punda na hali ya kuwatendea vitafanywa kupitia madaktari wa mifugo waliofuzu na kusajiliwa kwa kudadisi kuhusu
.
Matumizi ya punda
· Aina ya mizigo
· Dhumuni la kubeba
· Matumizi ya mara kwa mara
· Jinsi ya kubeba
· Uwezo wa kubeba
· Njia watumiayo kupita
Malisho
· Chakula
· Maji
· Mengineyo
Ukaguzi wa afya ya wa nje
· Masikio
· Ngozi
· Miguu


Kuendeleza Malengo na Madhumuni
Washiriki wataendeleza mikakati ya kuendeleza malengo ya mradi na madhumuni kwa kufanikisha mikakati kwa kushirikiana na Asasai za Serikali, Mashirika ya Hiari na watu wengine wote kwa kuzunguka Wilayani kahama na kutoa matangazo ya kuhamasisha vipeperushi.

Wednesday, May 31, 2006

Cat With no shelter

One Eye Removed Cat

In Tanzania the Domestic Cats are tortured due to local believes of witchcrafts, peoples are killings,cut the head and suck the blood, dig down live for the bussineess or lucky purposes or any other means of cruelty.

The Voice and eyes of cats during the night bring people in that believes. the real stories is that most of the people have no Animal Behaviour Education and non compassionate citizen .

we need to educate the Tanzania Citizens to be able to care and love cats and all animals

we believe that animals as living creatures are entitles to legal, moral and ethical consideration,
and have value more than economic measurements

Road Accident

On the high road called Morogoro Road this dog was killied by moving vehicles, the body of that dog was staying on that place more than three days.

Dogs here are seen as object not as living creature, the cruelties and abuses and killings are more major problems facing the Dogs here in Dar es salaam and other parts of the Country

Road accidents

Front Side of our office

Kahama Donkeys Welfare Project KDWP

1. Kahama Donkeys Welfare Project {KDWP}

Project Coordinator: Yohana J.S. Kashililah
Targeted Populations: Kahama Residents
Date of Starting: September 2006
End Date: February 2007


1.1 Project Description

Tanzania Animals Protection Organization {TAPO} will carry out the Kahama Donkeys Welfare Project in the Kahama District, situated 221 Km from Shinyanga town in the mainland of the United Republic of Tanzania.

The target population is Kahama Residences with their Donkeys in all 33 rural areas, with total population of about 399.000 residences. Of these about 60% owning donkeys will be participating in promoting the welfares of their Donkeys in their rural areas.

There are more than 1000 donkeys populations at Kahama {Report of 2001 Livestock’s Sensor}, with no veterinary clinic services available, 80% of residences are dealing with farming practise, 60% of farmers are owning the Donkeys, range 1 to 4 per single family.

Topographical features of Kahama District are, Mountains highlands with sand and-stone, with rocks scattered more spaces, and there is more than 13 villages


Donkey are recognized as en route to deliver practical, effective and suitable socio-economic assistance for the poverty reduction among the peoples of kahama, in general are very important in Transport and Agriculture works.


The load- carrying abilities of kahama donkeys are legendary sometimes exploited.
They are loaded with excessively heavy burden, carrying 100% of their body weight for long distances, the weight all in one narrow without means of saddle, whereby most of the people hang loads over the back of donkey without any saddle {e.g. two water drums linked only by cords, this put pressure directly over the backbone, frequently collapse en route, weak from hunger and thirst.

Donkey carts of Kahama is composed of a single shaft and pair of donkeys carry the weight on the draw pole through narrow neck straps or rope, also the draw carts Donkeys are usually in oxen yokes which put the weight on their long thin necks, inflicting severe strain and injury, and the ropes frequently interfere with their breathing. These are the major causes of the donkey discomfort and sores.
Most Donkeys are kept for Transport, whether pack transport or pulling carts through purpose of load Farm produce, firewood, water, manure, hire and building Materials
The farm produce means of Transport is the leading one used mainly by farmers during the Planting and harvesting seasons in many rural areas of Kahama whereby the farms are situated in difference kilometers from farmer residences, it will take about 8 hours per day, and even during the night donkeys are working, passing on road covered with rocks and on some mountain terrace. Including bad designing for carts and harnessing is a major problem cause of injuries of the kahama Donkeys, which are caused by donkey to pull from the neck rather than the chest

Most Donkeys conditions is weak from the body physically appearances to health status; most have presence of body lesions especially around the neck, chest, under the tail, on the front and back limbs, on the lower fore and upper fore, hooves have lesions and overgrowth


The Donkeys owners value their donkeys for load carrying and also the planting of farms, and other works, so there shall be given Donkey welfare education through the followings strategies.

Training and working practices
There is full information on good working practices with donkeys and farmers may work their animals to the point of stubborn refusal to work further, good training is also beneficial for general case of working if it includes complete control and commands, improved practices, and there shall be 3 days training class per single rural area, as follows

1. Training concerning Donkey shelters
This training will cover providing good shelter which is suitable for their donkey for all seasons of the year, due to the no waterproof coat of donkey, the shelter will protect donkey during the winter, and give them shade in the hot days, and escape from the heat and flies.
2. Training concerning feeding of donkeys
This training will cover farmers to identify poisonous grass, providing balanced diet for their donkey, and to protect form over feeding diseases


3. Training concerning basic donkey health care
This training will cover farmers to observe their donkeys if there is sick or fit to work, or anything wrong before calling vet-doctor. Working in the cool of the early morning and evening Regular rests in shade and with water available, hooves trimmed.


4. Training concerning handling the donkey
This training will cover donkeys on pulling carts and pack load, how to minimize the lesion produced by carts and saddle modification
2. Project Goals
Kahama Donkeys welfare project {KDWP}, is responsible for promoting and protecting the health, safety, and welfare of all donkeys found at Kahama, the six months project will enhance the Kahama residents to understand donkeys and respect them as living being, with the following goals;

Creating, maintaining and promoting any donkeys issues relating to their well-being upon human beings

Understanding, appreciation, improvements, developments of the donkey welfare among the people of kahama

3. Urgency and Sustainability

It is necessary to do this project this time because Donkey welfare stigma is at present rampant within kahama communities. It is urgent because stigma elimination is a prelude to wide scale donkey’s welfare. Wide scale donkey’s welfare is essential for providing support and care in the implementation of all initiative.

At the end of the Project Kahama residences in their rural areas will have been built capacity to reduce stigma and implement donkey welfare and support activities.

4. Project Management
Kahama Donkeys welfare project {KDWP} will work closely with advices from Sokoine University of Agriculture, Ministry of livestock’s developments, kahama district council, and kahama veterinary officers, any other interested NGO. Others are local government’s authorities, news media and the public to produce a welfare- sound, widely- supported plan for implementation. The key elements of the project management structure are:

A Project Management Team: made up of Tapo members and staff, qualified registered veterinary doctors, will conduct the day-to-day project management, following work plan, schedule and budget, ensure that there is adequate coordination with other project participants and other interest groups.

A Technical Advice Team” is made up professors from faculty of Veterinary Medicine of Sokoine University of Agricultures, Vet- Doctors from ministry of livestock’s Development.

5. Project Activities and Timeline

The project is expected to take six months and cost approximately
$ 17.340/ {the kahama donkey welfare project will include the following elements.

1. Analyze existing conditions

A detailed analysis of existing, donkey health, and treatment conditions will be conducted through qualified veterinary Doctors and question about:
Donkey uses;

Types of load,
Any saddle/harness,
Fit for harness,
Tethering,
Purpose of load,
Frequency use,
Terrain covered.

Husbandry and Management:

Feed,
Water,
Other

Physical Health Check up of
· Skin
· Ear
· Eyes
· Musculoskeletal
2. Develop Project Goals and Objectives
The participants will develop a strategy for developing project goals and objectives for the Kahama Donkey welfare project; a successful strategy will incorporate extensive work with any Government’s institutions, foreign NGO, news media, public involvement and any other individual. By moving around Kahama with advertising equipments, brochures, leaflets and posters shall be used

6. Opportunities for public Education and Outreach

Activity No.1 & 2

Kahama Donkey welfare project will produce 90% in Swahili language and 10% English language, and provides the following educational materials for free, brochure, leaflets, posters. {Dvds, Cds and videocassettes T-shirt, and caps will be sold to fundraising the project}. Whereby there will be five participants, using one hired vehicle to promote donkey welfare all around Kahama by using loud speakers and other advertising equipments.

Activity No. 3

Qualified veterinary Doctors will conduct this activity
Communication with input from community and interested organization will be achieved using.
· Training workshop
· Public meetings
· A website
· Paper newsletter
· Presentation

7. Risk

We believe the project can be delivered in the time scale envisaged and within the proposed budget. The duration of six months for the activities within kahama communities is adequate to bring about initial changes in knowledge, attitudes and practices of all Donkeys.

The main risks that may delay or reduce the effectiveness of this project are.
The poor attending of Donkeys owner in the training class in their rural areas, the project will take special effort to encourage donkey’s owners to participate in this project through local governing authorities.
Voluntarism is the cornerstone of this project. Dependence of voluntarism at local level to participate in this project will planned, executed and evaluated by the assistance form local governing authorities
Understanding of targeted population on training class through their types of background education status.
Culturally women have limited power In decision making in the communities, while they are main generator of family income, we will use rights based approach to sensitise both women and men

Wednesday, May 24, 2006

Wanyama

WANYAMA
Duniani kuna aina nyingi sana ya viumbe kama vile ndege, wanyama, samaki, wadudu na wengineo, na viumbe wote hao wanatabia , maumbile,mahitaji mapendo na mifumo mbalimbali ya kuendesha maisha mbali ya msaada wa binadamu kwa asili ya maisha ya viumbe wa duniani. Pia kuna wanyama ambao wana akali ya kutambua na kufanya vitu mbalimbali karibia kabisa na binadamu, na sifa kubwa zaidi kwa viumbe wengi ni kuwa wanalea na kuwatunza watoto wao.


Haki za Wanyama

Nini maana ya haki za wanyama?

Haki za wanyama maana yake wanyama wana aina Fulani ya kufikirika, kuthaminika—kufikirika, kuthaminika kutokana na nini bora kwa mapenzi, mahitaji, na maamuzi yao kutokujali kama hawasikii, wanatumiwa na binadamu, au wanakaribia kutoweka na kutokajali kama wanatunzwa na binadamu {kama ilivyo kwa binadamu aliyepungukiwa na akili anaayo haki hata kama watu wote hawampendi} ina maana kutambua kuwa wanyama siyo wetu kwa ajili ya chakula, kuvaa, kiburudisho, au majaribio ya kisayansi.

Ni Haki Zipi za Wanyama ?
Wanyama wanahaki ya kuthamiwa kwa maamuzi yao wenyewe kwa mfano, mbwa ana maamuzi ya kutokuwa na maumivu anayoyapata pasipo kuwa na sababu yeyote ile, maana, kwa hiyo tunalazimika kuchukua maamuzi yao katika kuwathamini na kuwajali mbwa kuwa na haki ya kutokuwa na maumivu yasiyo ya lazima anayoyapata.

Hata hivyo wanyama kawida hawana haki zinazofanana na binadamu, kwa sababu maamuzi na mahitaji yao kawida hayafanani na yetu, na baadhi ya haki zinaweza kuwa kinyume na maisha ya wanyama, kwa mfano, mbwa hana maamuzi, hafahamu haki ya kupiga kura na kwa hiyo hana haki ya kupiga kura, tangu hapo haki hiyo itakuwa haina maana kwa mbwa na kama ilivyo kwa mtoto.

Umesimama Wapi?
Kuna baadhi ya bianadamu ambao kwa huruma na upendo wanaweza kusimama na kumtoa jongoo barabarani na kumpeleka sehemu salama. Kujali matatizo na kuwajibika ni maadili yanayopanuka na tunalazimika kuishi kila siku kwa kuhukumu na kuhukumu kuamua kila kitu kinachotokea kwa ubaya na uzuri kama tunavyoweza.

Hatuwezi kuzuia mateso yote, lakini haina maana kuwa hatuwezi kuzuia mateso yeyote katika maisha ya sasa ya duniani yenye muenekano wa mapungufu ya uchaguzi, kawaida huwa kuna huruma na ubabe, njia ambazo wengi wetu tunazotumia katika kula, kuvaa, kuburudika, na kujifunza sisi wenyewe kuliko kuua wanyama.



Vipi Miti na Mimea?
Hakuna njia inayoonyesha tuamini kuwa miti na mimea inahisi maumivu, kwani haina mishipa ya fahamu “ubongo”na mwisho wa mishipa ya fahamu. Sababu pekee inayoonyesha kuwa wanyama wanahisi maumivu ni jinsi watakavyo jihami.
iwapo utashika kitu ambacho kitakuumiza au kujeruhi, maumivu yatakufundisha kutokugusa na kukiacha pekee siku nyingine. Tangu hapo miti na mimea haiwezi kutembea kuepuka maumivu na hivyo haitaji kijifunza kuepuka baadhi ya vitu.

Imani Katika Haki Za Wanyama
Ni vizuri kuamini katika haki za wanyama kwani kila mtu anawajibika katika maamuzi yake, lakini “uhuru wa kufikiri” kawaida huwa hauwendani na “uhuru wa kutenda”. Upo huru kuamini chochote unachotaka ingawaje huwaumizi wengine, unaweza kuamini kuwa wanyama ni lazima wauwawe, kwamba watu weusi ni lazima wawe watumwa, au mwanamke ni lazima apigwe, lakini hufanyi imani yako uiweke kwenye majaribio- yaani kwa kutenda.

Wanyama hawazielewi haki zao, mara nyingi hawaheshimu haki zetu, je ni kwanini tunatoa mawazo yetu ya kiroho juu yao?
Kwa sababu wanyama kushindwa kufahamu na kuingia katika miongozo yetu ni sawasawa na mtoto mdogo au kichaa kushindwa kufana hivyo. Wanyama hawako, hawana, au hawajawezeshwa kuchagua kubadilishwa tabia zao, lakini binadamu anayo akili ya kuchagua kati ya tabia zinazowaumiza wengine na kutokuwaumiza wengine.

Ni vigumu kuepuka kutesa wanyama na mara nyingi hufanyika bila kufahamu?
Ni kweli ni vigumu kuishi maisha yako bila ya kuleta majeruhi kwa viumbe wote, kwa bahati mbaya tumeshakanyaga siafu na viumbe wengine, lakini haina maana kuwa tumedhamilia kuwakanyaga siafu hao. Lakini kwa sababu unaweza kusababisha ajali kwa kumgonga mtu na gari haina maana kumfanya bianadamu awe ni kwa ajili ya kugongwa na gari.

Vipi kuhusu mila, tamaduni, na kazi zinazotegemea kutumia wanyama?
Uanzishaji wa magaari, uzuiaji wa biashara ya utumwa, na mwisho wa vita kuu ya pili ya dunia kulilazimisha kutokea na mifumo mingine ya kufanya kazi na kuiendeleza. Hii ilikuwa ni chachu katika maendeleo jamii za binadamu—siyo sababu ya kuvuruga maendeleo.

Wanyama wengi wanaotumika kwa chakula, kazi, manyoya, ngozi na majaribio ya kisayansi wamezaliwa kwa ajili hiyo?
Kwa kuzaliwa kwa shughuli hiyo hakuwewzi kubadilisha uwezo wa kibaolojia wa mnyama kusikia maumivu na huzuni.

Mungu ameweka wanyama hapa duniani kwa ajili ya kuwatawala, vitabu vya dini vimetupa utawala juu wanyama?

Kutawala siyo sawasawa na kutawala kwa mabavu na utesaji, mfano, Rais wa Tanzania anatawala au anawaongoza watanzania, lakini haina maana kuwa anaweza kuwala au kuwatesa watanzania. Iwapo tunatawala wanyama, ukweli kabisa ni kuwalinda, siyo kuwatumia kwa mahitaji yetu. Hakuna chochote kwenye vitabu vya dini kinachoweza kuelezea maisha yetu ya sasa na mipangilio ambayo inaharibu mazingira, kuharibu na kutokomeza vizazi vya wanyama wa porini na vifo vya wanyama kila mwaka.

Je ni kweli wanyama wanaofungiwa muda wowote hawateseki kwa sababu hawajui kitu chochote kile?
Kuzuiwa kufanya karibia vitu vyote vya asili kitabia kunasababisha maumivu au usumbufu wa hali ya juu hata kama mnyama amefungiwa tangu azaliwe anahitaji kutembea, kugusana pamoja kunyoosha miguu yao au mabawa yao na mazoezi. Wanyama wanaochungwa, na wanyama wanaotembea kikundi huwa wanapata kuchanganyikiwa wakati watakapoishi kwa kutenganishwa au watakapowekwa kwenye makundi makubwa ambapo wanashindwa kutambuana.

Iwapo utumiaji wa wanyama ungekuwa ni makosa ingekuwa ni uvunjaji wa sheria?
Utawala wa sheria siyo kinga ya imani ya kiroho, nania ametenda kosa na nani hakutenda kosa kisheria huamuliwa na maoni na mapendekezo ya wanasheria wa sasa, sheria zinabadilika kama mapendekezo ya jamii au mabadiliko katika siasa yatabadilika, lakini maadili hayabadilki. Angalia baadhi ya vitu ambavyo kwa wakati Fulani ilikuwa ni sheria dunia ajira ya mtoto, utumwa wa binadamu, na ukandamizwaji wa wanawake.

Wanyama hawana akili au wameendelea kama binadamu?
Kuwa na uwezo na akili nyingi hakumaanishi binadamu mmoja kumnyanysa mwingine kwa malengo yake, kwanini binadamu mwenye akili anyanyase wasio kuwa bindamu. Kuna wanyama ambao wana akili, wabunifu, wanaojali, wanaowasiliana na wenye uwezo wa kutumia lugha kuliko baadhi ya bianadamu , kama ilivyo kwa sokwe mtu akilinganishwa na mtoto mchanga au kichaa wa hali ya juu sana, je itakuwa wanyama wenye akili kuwa na haki na binadamu wenyekili kidogo kunyimwa haki?

Monday, May 22, 2006

Organization Profile

TANZANIA ANIMAL PROTECTION ORGANIZATION
Ubungo River Side, P.O.Box 62921 Dar Es Salaam, Tanzania
Tel; +255 0746 027419, +255 0764 499836.
Email, tap_org@yahoo.com

ORGANIZATION PROFILE


Tanzania Animals Protection Organization (TAPO), a registered non-government organization with registration No. 00NGO/0777.

The following are our Mission, Vision, Aims, and Objectives.

MISSION: To protect all Animals from Tortures, Cruelty, Abused, Diseases and killings in the country of Tanzania.


2. VISION; All Animals shall be respected as living beings like human beings.

3. AIMS: Our aims are to foster and promote the compassionate to Animals improvement and development of any matter concerning the protection of Animals. Understanding and appreciation of the Animals among the people of Tanzania without getting any profit.

OBJECTIVES:

To promote respect and compassionate for Animals through our activities, campaigns, public and school educational programmed.

To transform the way Animals are treated and perceived by human.

To make enforcement of existing Animals laws and anti-poaching campaigns.

To promote vegetarianism as the healthier life of eating.

To build Animals homes, Shelter, sanctuary.

To prevent unwanted and over population Animals and birds through our neutering and out reach programmed.

To see condition in Animals auction marts, Zoos, poultry farms, Animals breeders and people houses.

To provide wildlife conservation education in schools and public

To develop and deliver practical advises on the prevention and control of noticeable and endemic diseases in Tanzania livestock’s and other animals


.

.OUR BELIEVE

We believe that, Animal as living creatures are entitles to legal protection, moral and ethical consideration and have value beyond economic measurement.